MUNICH, Ujerumani
MKURUGENZI wa Bayer Leverkusen, Rudi Voller, amesema kuwa ana uhakika wa watamwekea ngumu nyota wake, Javier Hernandez endapo kama kuna timu yoyote itajitokeza kutaka kumsajili.
Kwa sasa Chicharito anahusishwa na timu za Sevilla na Valencia lakini Voller juzi aliliambia gazeti la Bild wanaendelea vizuri naye tangu alipowasili na hivyo hawana mpango wa kumwachia.